Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

TAASISI YA USULUHISHI WA MALALAMIKO NA TAARIFA ZA KODI

"Haki na Usawa"

Wajibu

Mamlaka Yetu

Taasisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi ni ofisi huru na isiyo na upendeleo ambayo itaendesha ofisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi chini ya Wizara ya Fedha na kuripoti kwa Waziri wa Fedha. Taasisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi itawajibika kupitia malalamiko yanayohusiana na huduma kuhusu Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kuzingatia Mkataba wa Huduma za Mlipakodi kama ulivyowekwa na TRA kuhusu masuala ya huduma. Taasisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi itakuwa ngazi ya mwisho ya mapitio katika mchakato wa utatuzi wa malalamiko ya TRA.