Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

TAASISI YA USULUHISHI WA MALALAMIKO NA TAARIFA ZA KODI

"Haki na Usawa"

Misingi Mikuu

Maadili ya Msingi

Maadili ya msingi yanafafanua utu wetu na yanatumika kama msingi wa kitamaduni wa taasisi hii. Haya ni mamlaka na ahadi zetu za msingi za uendeshaji wa shughuli zetu kwa wadau wetu

1. Uhuru

  • Tunafanya kazi chini ya Mamlaka ya Mapato Tanzania

2. Haki

  • Tunatenda kwa usawa na haki

3. Usiri

  • Tunafanya mawasiliano yote na wadau wetu kwa usiri mkubwa kwa kufuata kanuni zinazosimamia jukumu hili adhimu.

4. Uwazi

  • Tunahimiza uwazi katika mchakato wote  wa kusuluhisha malalamiko yoyote  yanayowasilishwa

5. Kuaminika

  • Sisi ni waaminifu, tunaaminika na kutegemewa

6. Weledi

  • Tumejitolea kufuata kiwango cha juu cha ujuzi, maarifa na umahiri katika kufikia majukumu yetu