Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

TAASISI YA USULUHISHI WA MALALAMIKO NA TAARIFA ZA KODI

"Haki na Usawa"

Upatanishi

Baada ya malalamiko kupokelewa, yatafanyiwa uchambuzi wa awali ili kubaini kama yanakidhi vigezo vya kushughulikiwa na Ofisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi. Endapo yatakidhi vigezo hivyo, yatasajiliwa rasmi kwa ajili ya hatua za uchunguzi na usuluhishi.

Ofisi hutumia njia mbalimbali za utatuzi, ikiwemo:

  • Usuluhishi (Conciliation);
  • Upatanishi (Mediation); au
  • Njia nyingine Mbadala za Utatuzi wa Migogoro (Alternative Dispute Resolution – ADR).